Wema afikishwa mahakamani

0
1820

Msanii wa filamu nchini, Wema Sepetu amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es salaam kusomewa makosa yanayomkabili ya kusambaza picha zisizo na maadili kwenye mitandao ya kijamii.

Habari zinasema kuwa Wema amefikishwa mahakamani na Mamlaka ya  Mawasiliano Nchini (TCRA).

Hivi karibuni Wema aliwaomba radhi mashabiki wake pamoja na Watanzania wote kufuatia kusambaa kwa picha zake hizo  ambazo hazina maadili zilizosambaa katika mitandao mbalimbali ya kijamii.