Miss Tanzania kutumia lugha ya kiswahili

0
2012

Mrembo wa Tanzania kwa mwaka 2018 Queen Elizeberth Makune amesema kuwa atatumia lugha ya kiswahili kwenye shindano la kumtafuta mrembo wa dunia pamoja na kutangaza vivutio mbalimbali vya utalii ili kuwavutia watalii wengi kutoka nchini China kuitembelea Tanzania.

Akizungumza jijini Dar es salaam baada kupewa tuzo ya pongezi na Chuo Cha Uhasibu ambapo yeye ni mwanafunzi wa mwaka wa tatu, Queen Elizeberth amesema kuwa amejiandaa vizuri ili kurejea na taji la dunia.

Miss Tanzania huyo wa mwaka 2018, – Queen Elizeberth , ametembelea Chuo hicho cha Uhasibu kwa lengo la kuwapa Wanafunzi moyo wa kusoma na Wafanyakazi wa chuo hicho moyo wa kufanya kazi kwa bidii.

Mrembo huyo anatarajiwa kuondoka nchini Ijumaa wiki hii kuelekea nchini China kushiriki shindano la urembo la dunia litakalofanyika Disemba nane mwaka huu