Makamu wa Rais ataka bajeti kuadhimisha urithi wetu

0
2427

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan amewaagiza wakuu wa mikoa nchini kutenga bajeti kwa ajili ya kuadhimisha tamasha la urithi wetu ngazi ya mkoa ifikapo mwezi Septemba kila mwaka.

Amesema hayo katika uzinduzi wa tamasha hilo kitaifa jijini Dodoma, ambapo pia amewaagiza wakuu wa mikoa kuishirikisha sekta binafsi katika maadhimisho ya tamasha hilo.

Makamu wa Rais ameiagiza Wizara ya Mali Asili na Utalii kulitangaza tamasha hilo kisheria na kutenga eneo maalum kitaifa kwa ajili ya tamasha hilo.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Japhet Hasunga amebainisha kuwa mchango wa sekta ya utalii katika pato la taifa bado hautoshelezi.