Cosby ahukumiwa kifungo jela kwa udhalilishaji

0
2359

Mahakama moja huko Pennsylvania nchini Marekani imemuhukumu kifungo cha kati ya miaka mitatu na kumi jela mchekeshaji Bill Cosby kwa kosa la udhalilishaji.

Cosby mwenye umri wa miaka 81, pia ameorodheshwa kuwa mtu mwenye tabia ya udhalilishaji kwa kuwa amekua akitenda vitendo hivyo mara kwa mara.

Wakati kesi yake ikiendelea, mchekeshaji huyo alikataa kuongea chochote licha ya kupewa nafasi ya kufanya hivyo.

Mwezi Aprili mwaka huu wakati kesi hiyo ikisikilizwa, Cosby alikutwa na hatia ya makosa matatu ya udhalilishaji kwa kumpatia kilevi na kumdhalilisha Andrea Constand mwaka 2004.
Ombi la Cosby la kutaka kuachiliwa kwa dhamana akisubiri kusikilizwa kwa rufaa yake limekataliwa.

Mchekeshaji huyo alitapa umaarufu miaka ya 1980 aliposhiriki katika kipindi cha televisheni kuhusu familia ya Kimarekani yenye asili ya Afrika iliyokuwa ikiishi Brooklyn, New York, umaarufu uliofikia kupewa jina la America’s Dad.