Basata yakanusha kuwafungulia wasanii Diamond na Rayvan

0
1294

Baraza la Sanaa la Taifa(Basata) limekanusha kuwafungulia wasanii wa muziki wa kizazi kipya Naseeb Abdul maarufu kama Diamond Platnamz na Raymond Mwakyusa maarufu kama Rayvan kufanya maonesho ndani na nje ya nchi .

Taarifa iliyosambazwa leo Decemba 22 iliyoandikwa na kaimu katibu wa Basata Onesmo Kayanda imesema kuwa baraza halijatoa ruhusa kwa msanii huyo na uamuzi wa awali unabakia kama ulivyo.

“Baraza liasisitza kwamba halijawafungulia wasanii hao kufanya onesho lolote ndani nan je ya nchi kama taarifa zinavyosambazwa”alisema Kayanda katika taarifa ya Basata.
Tarehe 18/12/2018 Basata iliwafungia wasanii hao kujishughulisha na sanaa ndani na nje ya nchi kwa kipindi kisichojulikana kutokana na kutumia kwa makusudi wimbo wao wa Mwanza ambao uemfungiwa na Baraza la Sanaa kwa sababu za kimaadili.

Aidha Basata imesisitiza kuwa linawataka wasanii hao kutii maagizo waliyopewa na kuacha mara moja kupotosha umma kwa kusambaza taarifa za uongo kabla ya hatua kali Zaidi kuchukuliwa Zaidi yao.