Wanawake wapatiwa mafunzo ya ujasiriamali

0
1672

Wanawake 150  wajane na wanaoishi katika mazingira magumu katika wilaya ya Temeke jijini Dar Es Salaam wamejikwamua kiuchumi kupitia mradi wa kuwajengea wanawake uwezo wa kiuchumi –IWAPOA.

Akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo ya ujasiriamali kwa wanawake jijini Dar Es Salaam, Meneja mradi huo Vivian Komba amesema baadhi ya wanawake hao wameanzisha shughuli za ujasiriamali na wengine wamejiunga katika vikundi vya kifedha- VICOBA.

Amesema mradi huo umetekelezwa katika kata sita za wilaya ya Temeke na wanawake hao wamepewa mafunzo ya jinsi ya kuanzisha shughuli za ujasiriamali na kazi za mikono.