Wajasiriamali wadogo Tanga wapatiwa vitambulisho

0
1612

Mkuu wa mkoa wa Tanga, -Martine Shigela amewaagiza Wakuu wa wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri za mkoa huo kuwasimamia wafanyabiashara wadogo katika maeneo yao ili wasibughudhiwe na suala la ulipaji kodi usiozingatia utaratibu.

Shigela ametoa kauli hiyo wakati wa ugawaji wa vitambulisho maalum vya wajasiriamali wadogo, vitambulisho vilivyotolewa na Rais John Magufuli Disemba 10 mwaka huu.

Lengo la vitambulisho hivyo vilivyotolewa na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) ni kuwatambua wajasiriamali wadogo katika maeneo yote nchini.

Wajasiriamali wanaopatiwa vitambulisho hivyo, ni wale wenye biashara zenye mtaji usiozidi Shilingi Milioni Nne.