Wafanyabiashara waachwa nyuma kasi ya Magufuli uchumi wa viwanda

0
2065
Mkurugenzi Mtendaji wa TPSF Godfrey Simbeye

Taasisi ya sekta binafsi nchini TPSF imesema kuna umuhimu kwa wafanyabiashara kwenda na kasi ya serikali katika utekelezaji wa sera ya uchumi wa viwanda ili sera hiyo iweze kuwa na tija kwa taifa.

Akizungumza katika kikao cha sekta binafsi jijini Dar es salaam Mkurugenzi Mtendaji wa TPSF Godfrey Simbeye amesema serikali inakwenda haraka kuliko sekta binafsi jambo ambalo halitakiwi.

Baadhi ya washiriki wa taasisi za sekta binafsi zinazosimamia wafanyabiashara wamesema vikao kama hivyo vinawapa nguvu ya kuwa na sauti moja wanapokabiliana na serikali kwa maslahi ya wafanyabiashara.