TRA watakiwa kuwajengea wafanyabiashara tabia ya ulipaji kodi kwa hiari

0
1279

Mkuu wa Mkoa wa  Mbeya, Albert Chalamila amewataka wafanyabiashara mkoani humo kujenga tabia ya kulipa kodi kwa hiari na kuwatahadharisha baadhi ya maafisa wa Mamlaka ya Mapato nchini  -TRA wanaotumia mianya ya kujinufaisha kwa kuchukua fedha nje ya utaratibu  wa serikali kuacha mara moja.

Chalamila ametoa rai hiyo Mkoani Mbeya baada ya  kuzungumza na baadhi ya wawekezaji na wafanyabiashara kuhusiana na changamoto zinazowakabili na namna ya kuzitatua.

Amesema moja ya mikakati ya uongozi wa Mkoa wa Mbeya ni  kuhakikisha  wawekezaji wanajengewa uwezo na mazingira mazuri ili  waweze kulipa kodi.

Ameongeza kuwa lazima kuwepo na mahusiano ya moja kwa moja   kati ya mfanyabiashara na serikali yatakayowezesha kwa pamoja kufikia malengo ya kuinua uchumi nchini.