TADB yasema ina mtaji wa kutosha

0
2501

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Nchini (TADB) Japhet Justine amesema kuwa benki hiyo ina mtaji wa kutosha kwa sasa kwa ajili ya kuwahudumia wakulima.

Justine amesema kuwa kwa mujibu wa upembuzi uliofanywa mwaka 2011 wakati wa mchakato wa kuanzisha TADB, mtaji unaohitajika kwa ajili ya kuiwezesha benki hiyo ifikie malengo yake na kutimiza matarajio ya serikali na wakulima ifikapo mwaka 2035 ilikuwa ni Dola Milioni mia Tano za Kimarekani ambazo ni sawa na Shilingi Bilioni 800.

Amefafanua kuwa tangu kuanza shughuli rasmi za ukopeshaji mwaka 2015, serikali imekuwa ikiendelea kuipatia benki hiyo mtaji.

Hadi kufikia mwisho wa mwezi wa Julai mwaka 2018, Benki ya Kilimo imetoa mikopo ya zaidi shilingi Bilioni 48.6 ikiwa ni ukuaji wa shilingi Bilioni 37.2 katika kipindi cha miezi saba ya mwaka 2018.

Mikopo hiyo imewanufaisha zaidi ya wakulima Laki Tano na Ishirini Elfu.