Serikali yakerwa na watu wanaofanya vitendo vya utoroshaji madini

0
1388

Naibu  Waziri wa Madini  Stanslaus  Nyongo amesema vitendo vya utoroshaji wa madini nje ya nchi vinavyofanywa na baadhi  ya wachimbaji wadogo vimesababisha serikali kukosa mapato.

Akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo ya usimamizi endelevu wa rasilimali madini kwa wachimbaji wadogo wa Bati Wilayani Kyerwa Mkoani Kagera Naibu  Waziri  Nyongo amesema hali hiyo imesababisha wingi wa wachimbaji kutolingana na mchango wao katika pato la taifa.

Katika mafunzo hayo inaelezwa kuwa idadi ya wachimbaji wadogo wa madini ni Asilimia tisini na sita ya wachimba madini wote nchini lakini huchangia Asilimia nne tu katika pato la taifa kutokana na sababu kadhaa ikiwemo baadhi yao kutorosha madini.

Baadhi ya wachimbaji wadogo wa madini ya bati wanaelezea matarajio yao baada ya mafunzo hayo kutokana na changamoto wanazokabiliana nazo.

Mafunzo hayo yameandaliwa na Wizara ya Madini  kwa kushirikiana na Shirika la Madini nchini -Stamico pamoja na Wakala wa Jiolojia.