NSSF kukuza uhusiano na benki za NMB, CRDB na UBA

0
2648

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa ya Hifadhi ya Jamii (NSSF) William Erio amekutana na kufanya mazungumzo na menejimenti za Taasisi Tatu za kibenki nchini ambazo ni NMB, CRDB na UBA.

Lengo la mkutano huo uliofanyika jijini Dar es salaam ni kuendeleza na kukuza uhusiano wa kibiashara baina ya NSSF na benki hizo tatu.

Wakati wa mkutano huo masuala mbalimbali yamejadiliwa ambayo lengo lake ni kuimarisha ushirikiano utakaowezesha kukuza maendeleo katika sekta ya uchumi kupitia benki za NMB, CRDB, UBA na shirika hilo la Taifa la Hifadhi ya Jamii.

Wakurugenzi waliokutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, -William Erio ni Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya CRDB, – Charles Kimei, Usman Imam Isiaka ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya UBA pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa benki ya NMB, – Ineke Bussemaker