MCB yaanzisha huduma ya mikopo ya dharura

0
2001
Mkuu wa kitengo cha ukuzaji biashara na masoko wa benki ya MCB Valence Luteganya (wa tatu kushoto) akiongea na waandishi wa habari katika uzinduzi wa huduma mpya ya benki hiyo ya Mikopo ya dharula.

Benki ya Biashara ya Mwalimu (MCB) imeanzisha huduma ya mikopo ya dharura ambayo rejesho lake hukatwa kwenye mshahara wa mteja (Salary advance) kwa lengo la kumwezesha mteja kuyakabili mahitaji muhimu yanayojitokeza wakati wowote.

Mkuu wa kitengo cha ukuzaji biashara na masoko wa benki hiyo Valence Luteganya amesema huduma ya ‘Salary Advance’ inawahusu wateja wafanyakazi wanaopitisha mishahara yao katika benki ya mwalimu ambao wataweza kupata mkopo wa hadi asilimia 50 ya mishahara yao.