Marekani yatishia kujiondoa WTO

0
3304

Rais Donald Trump wa Marekani ametishia kuiondoa nchi yake kwenye Shirika la Biashara Duniani (WTO) iwapo shirika hilo litashindwa kubadilisha utendaji wake kwa nchi hiyo.

Mara nyingi Rais Trump amekuwa akidai kuwa WTO imekua haitendi haki kwenye maamuzi yake dhidi ya Marekani na kwamba imekua ikifanya kazi zenye manufaa kwa nchi mbalimbali isipokua kwa nchi hiyo.

Shirika hilo la Biashara Duniani lilianzishwa kwa ajili ya kusimamia sheria za biashara duniani na kutatua tofauti za kibiashara kati ya nchi na nchi.

Hivi karibuni Marekani ilipinga uchaguzi wa majaji wapya wa WTO ambao kazi yao ni kujadili masuala ya kibiashara ya nchi mbalimbali na hatimaye kuyatolea maamuzi.