IITA yasisitiza uzalishaji wa dawa ya Aflasafe

0
2340

 

Taasisi ya Kimataifa ya Kilimo cha Kitropiki (IITA) imeanza kuwasisitiza wawekezaji wa Tanzania kuanzisha viwanda vya uzalishaji wa dawa ya kupambana na Sumukuvu ijulikanayo kama Aflasafe ili kunusuru uharibifu wa mahindi na karanga.

 

Akizungumza  jijini Dar es salaam wakati wa mdahalo wa wawekezaji,  mtaalam aliyefanya utafiti wa kupatikana kwa dawa hiyo Steve Kisakye amesema kuwa  dawa ya Aflasafe ipo katika mchakato wa kusajiliwa na Taasisi ya Utafiti na Udhibiti wa Viuatilifu Tanzania (TPRI)  na imeshafanyiwa majaribio katika mikoa mbalimbali nchini.

 

Kwa upande wake afisa Kilimo Mkuu kutoka wizara ya kilimo Beatrice Pallangyo amewashauri wakulima nchini kutumia dawa hiyo ili kuepusha Sumukuvu inayoingia katika mazao hayo ya mahindi na karanga wakati wa mavuno na kuathiri afya za walaji.