Dkt Shein kufungua maonesho ya utalii Zanzibar

0
1993

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein anatarajiwa kufungua maonesho ya utalii yatakayofanyika Zanzibar kuanzia Oktoba 17 hadi 20 mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Unguja, Waziri wa Habari, Utalii na Mambo ya Kale wa Zanzibar, – Mahmoud Thabit Kombo amesema kuwa maonesho hayo yatahusisha takribani  kampuni 150 za utalii.

Amesema kuwa lengo la maonesho hayo kufanyika Zanzibar ni kutangaza utamaduni wa Mzanzibar na vivutio vya utalii vinavyopatikana visiwani humo.

Waziri Kombo ametaja nchi zitakazoshiriki maonesho hayo kuwa ni pamoja na Lebanon, China,  Indonesia, Malaysia , nchi za falme za kiarabu na nchi za masharikai ya kati.