Wachimbaji madini wasisitizwa kutunza mazingira

0
110

Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Hemed Suleiman Abdulla ametoa wito kwa wachimbaji madini nchini kutunza mazingira wakiwa kwenye shughuli zao ili kutoathiri viumbe hai.

Abdulla ameyasema hayo wakati wa ufungaji wa maonesho ya Sita ya Kimataifa ya Teknolojia ya Madini mkoani Geita.

“Kama tunavyofahamu shughuli za madini ikiwemo uchimbaji na uchenjuaji zinaweza kuathiri mazingira. Natoa wito kwa wachimbaji wa madini hasa wachimbaji wadogo kuzingatia sheria, kanuni, taratibu na miongozo iliyowekwa na Serikali katika kuhakikisha shughuli za madini zinakwenda sambamba na utunzaji wa mazingira (miti, wanyama na vyanzo vya maji) ili kuwa na uchimbaji endelevu na salama kwa kizazi cha sasa na baadae.”‘-
Amesema Abdulla.