Hemed Abdulla : BOT endeleeni kununua dhahabu

0
134

Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Hemed Suleiman Abdulla ametoa wito kwa Benki Kuu ya Tanzania (BOT), kuendelea kununua dhahabu kwa lengo la kuiwezesha nchi kuwa na akiba ya dhahabu ya kutosha.

Abdulla ameyasema hayo wakati wa ufungaji wa maonesho ya Sita ya Kimataifa ya Teknolojia ya Madini mkoani Geita.

Mpaka sasa BoT imenunua kiasi cha kilogram 418 za dhahabu yenye kiwango cha asilimia 99.9. Na taarifa ya BOT iliyitolewa na Gavana wake ilieleza kuwa Benki Kuu itanunua dhahabu kutoka kwa wachimbaji wa ndani na wafanyabiashara wa dhahabu kwa fedha za Kitanzania.