WATAALAMU WA TEHAMA JESHI LA POLISI WATHAMINIWE

0
126

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Jumanne Sagini amelishauri Jeshi la Polisi Tanzania kutambua ujuzi, weledi na uzalendo wa wataalam wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika jeshi hilo kwa kuwapandisha vyeo mara kwa mara bila ya kuwaondoa kwenye fani zao.

Amesema ipo haja ya Jeshi hilo kuonesha kuwathamini kwakuwa wamekubali kuendelea kulitumikia jeshi hilo bila ya kutamani kwenda kufanya kazi kwingine licha ya kuwa na ujuzi walionao.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa mfumo wa kidijitali wa kifedha wa Jeshi la Polisi Tanzania ’URA Mobile’ iliyofanyika katika viwanja vya chuo cha Taaluma ya Polisi Dar es Salaam kilichopo Kurasini Dar es Salaam, Sagini ameongeza kuwa kwa taaluma waliyoionesha wataalamu hao wanastahili kuthaminiwa.

“Ndio maana nikamuambia IGP kwenye zile promotion promotion zile hawa wawapeleke harakaharaka ili maslahi ambayo angayatafuta kule ayapate huku.

Tabu yenu mkimpandisha akapanda sana mtamtoa IT mnamwambia simamia kamisheni, huyu mpandisheni alafu abaki palepale ilitaaluma yake na uwezo wake tuendelee kunufaika nao. Kuna dhambi gani mtu anafanya wonders mnampandisha anakuwa na licheo likubwa limshahara likubwa alfu anafanya kazi yake ileile ya taaluma maana huko nako tunawahitaji” Amesema Sagini