KIHENZILE AFANYA ZIARA BANDARINI

0
198

Naibu Waziri wa Uchukuzi David Kihenzile amefanya ziara yake ya kwanza toka ateuliwe kushika wadhifa huo kwa kutembelea na kukagua baadhi ya bandari zinazosimamiwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), ambapo amejionea namna shughuli mbalimbali zinavyoendeshwa.

Akiwa katika ziara hiyo Kihenzile amebainisha mambo kadhaa ambayo ni mikakati ya Serikali katika kuchochea kasi ya maendeleo nchini, kupitia bandari.

Mikakati hiyo ni pamoja na kujenga matenki makubwa yenye uwezo wa kuhifadhi mafuta hadi tani laki tatu na elfu sitini na usimikaji mtambo mkubwa wa kisasa Kigamboni, Dar es Salaam kwa ajili ya kupima kiwango cha mafuta kinachoingizwa kupitia bandari ya Dar es Salaam.

Wakati wa ziara hiyo Naibu Waziri wa Uchukuzi David Kihenzile pia amekagua eneo maalum linalotumika
kushusha magari kutoka kwenye meli ambapo kwa siku yanashushwa takribani magari laki tatu na eneo lenye uwezo wa kuhifandi magari elfu sita kwa wakati mmoja.