TRILIONI 1 KUBORESHA MIUNDOMBINU YA MIJI

0
165

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mohamed Mchengerwa, ameshuhudia utiaji saini mkataba wa utekelezaji wa mradi wa Uboreshaji wa Miundombinu ya Miji ya Tanzania (TACTIC), mradi utakaoziendeleza halmashauri 45 nchini.

Mradi huo utagharimu dola Milioni 410 za Kimarekani ambazo ni zaidi ya shilingi Trilioni Moja, fedha kutoka Benki ya Dunia.

Mradi huo utakaotekelezwa kwa muda wa miaka sita unalenga kuboresha miundombinu kwa kujenga barabara za lami, masoko, vituo vya mabasi, bustani za kupumzikia, mitaro ya maji ya mvua na vivuko.