Darasa la saba kuanza mitihani kesho

0
331

Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) limetangaza kuanza kwa mitihani ya kuhitimu elimu ya msingi itakayofanyika Septemba 13 na 14 mwaka huu, ambapo wanafunzi 1,397,370 wanatarajiwa kufanya mitihani hiyo, ikiwa na ongezeko la watahiniwa 13,000, sawa na asilimia 0.93 ikilinganishwa na mwaka jana.

Katibu Mtendaji wa NECTA, Dkt. Said Mohammed, amewataka watahiniwa kuwa waadilifu na kuacha vitendo vya ulaghai. Pia, ametoa wito kwa Watanzania kutoa taarifa pindi wanapobaini vitendo vyovyote vya ulaghai juu ya mitihani hiyo.

Katika mtihani wa kumaliza elimu ya msingi, jumla ya masomo sita yatatahiniwa, ambayo ni Kiswahili, Kiingereza, Sayansi na Teknolojia, Hisabati, Maarifa ya Jamii na Stadi za Kazi, pamoja na Uraia na Maadili.