Waajiri watakiwa kuzingatia usalama na afya mahali pa kazi

0
214

Wakala wa Usalama na Afya Mahali Pa Kazi (OSHA) imetakiwa kuhakikisha inaendelea kusimamia usalama na afya sehemu za kazi ili kuimarisha utendaji na afya kwa Wafanyakazi

Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Prof. Joyce Ndalichako wakati wa ufunguzi wa mafunzo elekezi kwa Wabunge wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti leo mkoani Arusha.

Prof. Ndalichako amesema masuala ya usalama na afya ni mtambuka na yanagusa sekta zote za uchumi, hivyo ni vyema kushirikiana ili kuimarisha mifumo ya usimamizi wa usalama na afya kwa wafanyakazi nchini.

Akizungumza awali, Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhandisi Cyprian Luhemeja ameishukuru kamati hiyo kwa kuishauri vyema serikali kuhusu masuala ya usimamizi wa usalama na afya mahali pa kazi na amewahakikishia ofisi hiyo itaendelea kusimamia kwa ufanisi masuala hayo.

Naye, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usalama na Afya Mahali Pa Kazi (OSHA), Khadija Mwenda amesema taasisi hiyo itahakikisha ustawi wafanyakazi unaimarika sambamba na kulinda uwekezaji kupitia mifumo ya usalama na afya sehemu za kazi