Lissu na wenzake mbaroni

0
251

Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Arusha, Justine Masejo amethibitisha kukamatwa kwa Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tundu Lissu na wenzake watatu kwa tuhuma za kufanya mikusanyiko isiyo halali na kuzuia askari kutekeleza majukumu yao.

Kamanda Masejo amesema baada ya mahojiano hayo na ukamilishwaji wa taratibu zingine, hatua nyingine za kisheria zitafuata.