Mifumo ya chakula na mazingira

0
255

Matukio mbalimbali katika picha wakati wa kikao kilichohusisha wadau wa mazingira kando ya mkutano wa Mifumo ya Chakula Afrika unaofanyika mkoani Dar es Salaam, ambao wamejadili mambo kadhaa ikiwa ni pamoja na mabadiliko ya Tabianchi na namna ya kukabiliana na changamoto zake.

Kikao hicho pia kimepokea maoni, mapendekezo na mchango kutoka Tanzania ambayo imewakilishwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Dkt. Selemani Jafo.

Miongoni mwa mapendekezo ya Tanzania ni kuyataka mataifa ya Afrika kuachana na kilimo cha mazoea na kuwekeza zaidi kwenye utafiti Ili kukabiliana na mabadiliko ya Tabianchi.