DAR na mkakati wa ujenzi wa vituo vya Polisi

0
160

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amesema mkoa huo umejipanga kujenga vituo vya polisi ili kutoa suluhu ya upungufu wa vituo hivyo kwa mkoa huo.

Kwa sasa Dar es Salaam ina vituo 128 vya polisi ambapo uhitaji ni 217, hivyo kusababisha upungufu wa vituo 89.

Chalamila amesema mkoa wa Dar es Salaam umejipanga kujenga vituo hivyo pungufu ambapo kila halmashauri itajenga vituo viwili ndani ya mwaka wa fedha 2023/2024.