Doto Cup yaleta msisimko Geita

0
171

Timu ya soka ya Butizya FC ya mkoani Geita imeingia hatua ya fainali baada ya kuifunga timu ya Runzewe Academy magoli 4 bila, katika michuano ya Doto Cup iliyofanyika katika uwanja wa mpira wa shule ya sekondari ya Ushirombo.

Mwemyekiti wa kamati ya mashindano ya Doto Cup Nelvin Salabaga amesema, ligi hiyo inayodhaminiwa na Mbunge wa jimbo la Bukombe ambaye pia ni Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko imekuwa na msisimko mkubwa na vijana wengi wamejitokeza kwa ajili ya kushiriki.

Baadhi ya wachezaji wamesema kucheza katika michuano ya Doto Cup kunaibua vipaji vyao na kwamba
watu wengi wanajitokeza kuwaangalia na wanatarajia kuchukuliwa kwenda kucheza sehemu zingine ambapo watapata ajira.

Tangu ilipoanzishwa mwaka.2016, Michuano ya Doto Cup imekuwa ikifanyika kila mwaka.