Rapa Kontawa asalimisha sare JWTZ

0
193

Rapa wa muziki wa Tanzania @kontawaa amejisalimisha Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), kurudisha mavazi ya Jeshi aliyokuwa akiyatumia.

@kontawaa amerejeshe mavazi hayo zikiwa zimepita siku chache baada ya JWTZ kuwataka Wasanii wanaotaka kutumia sare za Jeshi hilo kwenye kazi zao kufuata utaratibu wa kuomba kibali ili waruhusiwe kutumia mavazi hayo, huku likitoa siku saba kuanzia Agosti 24,2023 kwa Wananchi kusalimisha mavazi ya Jeshi au yanayofanana na sare za Jeshi.

Tangazo hilo la JWTZ lilitolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano Makao Makuu Luteni Kanali Gaudentius llonda.

“Tunatoa siku saba kuanzia leo iwe mwisho wa kuyavaa, kuyatumia au kuyauza, kwa wale Wasanii wao watafuata utaratibu wa kuomba kibali ili waruhusiwe kutumia mavazi hayo, baada ya siku saba atakayekutwa na mavazi hayo atachukuliwa hatua kali ambayo itakuwa fundisho kwa wengine,” Alionya Luteni Kanali llonda.