Maandamano Kuelekea Siku ya Kiswahili

0
147

Maandamo ya kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya Kiswahili Duniani ambayo Kitaifa yanafanyika Zanzibar Julai 07, 2023.

Matembezi hayo ambayo yamewashirikisha Wadau, Wanafunzi na Wabobezi wa lugha ya Kiswahili yameanzia shule ya sekondari ya Dkt. Ali Mohammed Shein na kuhitimishwa katika uwanja wa Ziwani Polisi mkoa wa Mjini Magharibi.

Leo unafanyika uzinduzi wa kilele cha maadhimisho ya Siku ya Kiswahili Duniani ambapo mgeni rasmi ni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.