Mwakinyo apoteza pambano Uingereza

0
204

Bondia Mtanzania, Hassan Mwakinyo amepoteza pambano dhidi ya bondia Muingereza Liam Smith kwa TKO raundi ya nne katika pambano lenye roundi 12 huko Liverpool nchini Uingereza.

Mwakinyo alianza pambano vizuri na wakati likiendelea alionekana kuumia mguu na kumlazimu mwamuzi kusimamisha pambano hilo.

Lakini hata hivyo kabla ya raundi ya nne kumalizika, Mwakinyo alionekana akipiga goti chini.