Mussa Idd Mussa wa TBC afariki dunia

0
330

Mfanyakazi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Mussa Idd Mussa amefariki dunia alfajiri ya leo  katika hospitali ya Taifa  Muhimbili mkoani Dar es Salaam,  alipokuwa akipatiwa matibabu.

Mwili wa Mussa ambaye alikuwa Mtumishi wa TBC,  utaagwa katika  hospitali ya Taifa  Muhimbili saa saba mchana hii leo.

Baadaye leo,  utasafirishwa  kwenda  nyumbani kwao Pangani  mkoani Tanga kwa ajili ya mazishi.

Mungu ailaze Roho ya Marehemu Mahali Pema Peponi Amina.