Volkano yalipuka tena Guatemala

0
2005

Kwa mara nyingine serikali ya Guatemala imewahamisha watu wanaokaa karibu na mlima wenye volkano hai wa Fuego nchini humo baada ya mlima huo kulipuka tena kwa mara ya pili wiki hii.

Hadi sasa watu 75 wamethibitika kufa na wengine mia mbili hawajulikani walipo baada ya mlipuko wa kwanza kutokea katika mlima huo na kusababisha mawe, matope ya moto na majivu kurushwa umbali mrefu kutoka kwenye mlima huo.

Habari zinasema lava na majivu yameanza tena kumwagika katika eneo linalozunguka mlima huo na zoezi la uokoaji wakati mwingine likikwamishwa na majivu pamoja na moshi unaoendelea kufuka.