Wadau wa elimu kupitia TBC kukutana Arusha Juni 17

0
2008

Waziri wa elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako

Mkutano wa wadau wa elimu kupitia Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) utafanyika Juni 17 hadi 23, 2018 katika ukumbi wa mahakama ya kimataifa (TANAPA) mjini Arusha.

Taarifa iliyotolewa na uongozi wa TBC imewataka wadau wote kulipa ada ya ushiriki katika mkutano huo ambayo ni kiasi cha Shilingi laki tano (500,000 /=) kwa kila mshiriki, mapema iwezekanavyo.

Taarifa hiyo imeelekeza kuwa malipo yanapaswa kufanyika katika ofisi za TBC makao makuu huko barabara ya Nyerere Dar es Salaam au TBC1 Mikocheni jijini au katika ofisi za Masoko zilizopo mtaa wa Zanaki Dar es Salaaam.

Taarifa hiyo imesema pia kuwa malipo yanaweza kufanyika kupitia akaunti ya benki ya CRDB namba 0IJ 1043002901 jina la akaunti likiwa ni TBC.

Watu walioko mikoani wameshauriwa kufanya malipo kupitia ofisi za kanda za TBC na kwa mawasiliano zaidi wanaweza kupiga simu namba 0738 681066.

Uongozi wa TBC unawataka wadau kuthibitisha ushiriki wao kabla ya Juni 15, 2018