Waziri Mkuu Kassim Majaliwa awahamasisha watanzania kununua Hisa

0
2049

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akinunua hisa toka kampuni ya Simu ya Vodacom

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amenunua Hisa za thamani ya shilingi milioni 20 za kampuni ya Simu ya Vodacom ili kuwahamasisha watanzania kuchangamkia fursa za uwekezaji kwenye masoko ya hisa na mitaji.

Akizungumza wakati akinunua Hisa hizo jijini Dar es salaam Waziri Mkuu amesema hisa za shilingi milioni 10 kati ya hisa hizo ni za kwake na na zinazobakia ni kwa ajili ya Mke wake Mary Majaliwa.

Wakizungumzia uwekezaji huo waziri wa Fedha na mipango Dokta Philip Mpango na katibu mtendaji wa baraza la uwezeshaji wananchi kiuchumi NEEC Beng’i Issa wamewataka wakulima na wafugaji kuwekeza kwenye Hisa ili waweze kunufaika moja kwa moja na ukuwaji Wa uchumi .

Vumilia Mwasha