Matatizo ya moyo yamuondoa Aguero kwenye soka

0
174

Nyota wa Argentina na Klabu ya Barcelona, Sergio Kun Aguero (33), Leo Disemba 15, 2021 atatangaza rasmi kustaafu Soka baada ya kugundulika kuwa ana matatizo ya moyo.

Sergio alijiunga na Barcelona akitokea Manchester City na pale Barca amecheza mechi 5 tu za msimu huu.

Aguero Leo anahitimisha safari yake ya soka akiwa amecheza mechi 786 na kufunga magoli 427.