Wajasiriamali kupatiwa mikopo yenye masharti nafuu

0
2482

Serikali imesema itaendelea kuboresha mazingira ya uwekezaji kwa kuwapatia mikopo yenye masharti nafuu kina mama na vijana. Akizungumza mjini Arusha katika hafla ya kukabidhi mikopo isiyokuwa na riba kwa kina mama wajasiliamali Waziri Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Jenista Mhagama amesema serikali itaendelea kuwasaidia wananchi ili waweze kujikwamua kiuchumi.

Pia ameahidi kuwasaidia wanawake kuanzisha umoja wenye nguvu utakaowasaidia kujikomboa kutoka katika umasikini.

Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amewaagiza viongozi wa ngazi ya chini katika mkoa huo kuhakikisha wanatatua changamoto zinazowakabili wananchi hao na kuwasaidia kujikwamua kiuchumi.

Zaidi ya Kinamama 600 wa mkoa wa Arusha wanatarajiwa kupewa mikopo isiyokuwa na riba yenye thamani ya shilingi milioni miamoja na ishirini.