68,019 kujiunga shahada ya kwanza

0
203

Waombaji  68,019  sawa na asilimia 73.2 ya waombaji  92,809, wamechaguliwa kujiunga katika Taasisi za Elimu ya Juu kwa kozi za Shahada za kwanza kwa mwaka wa masomo 2021/2022.

Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Tanzania (TCU) Profesa Charles Kihampa amesema ongezeko la waombaji limetokana na kuongezeka kwa wahitimu wa kidato cha sita.

Aidha Profesa Kihampa amesema dirisha la awamu ya pili la udahili linafunguliwa Agosti 24 mwaka huu hadi Septemba 6 mwaka huu, ili kutoa fursa kwa waombaji waliokosa nafasi kuomba katika awamu hiyo.

TCU imewataka waombaji kutuma maombi moja kwa moja katika vyuo, na kwa waombaji 35,548 waliochaguliwa chuo zaidi ya kimoja katika awamu ya kwanza ya udahili wanatakiwa kuthibitisha chuo kimojawapo katika vile walivyochaguliwa.mwisho