MAANDALIZI YA SHEREHE ZA MWAKA KOGWA

0
172

Maandalizi ya sherehe za Mwaka Kogwa zinazofanyika baadae hii leo yakiendelea katika uwanja wa Mwaka Kogwa, Makunduchi mkoa wa Kusini Unguja.

Sherehe hizo zinafahamika sana kama ni miongoni mwa mila za Kizanzibari na kwa sasa zinatambulika kuwa za Kitaifa.

Hufanyika kila mwaka  ambapo wageni kutoka ndani na nje wamekuwa wakihudhuria, na hivyo kuwa chanzo cha mapato.