Waziri Mkuu aongoza swala ya Eid al-Fitr kitaifa

0
314

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameongoza maelfu ya waumini wa madhehebu ya Kiislamu katika swala ya Eid Al-Fitr iliyofanyika kitaifa katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam.

Swala hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali na dini akiwemo Mufti wa Tanzania, Sheikh Abiubakar bin Zuberi na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Aboubakar Kunenge.

Akiwasilisha salamu za Rais wa Jamhuri ya Muungamo wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan na makamu wake, Dkt. Philip Mpango kwa waumini hao, waziri mkuu amesema viongozi hao wanawatakia Waislamu na Watanzania wote nchini sikukuu njema.

Ametumia jukwaa hilo kuwahisi Waislamu kusherehekea siku kuu ya Eid al-fitr kwa kuiishi miiko ya dini hiyo.

Awali, akihutubia maelfu ya Waislamu waliofika katika ibada hiyo, Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum amesisitiza umuhimu wa amani, upendo na kutosherehekea katika mazingira ya kupata dhambi.

Rais Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Baraza la Eid al-Fitr leo alasiri.