TANZIA: Maalim Seif Afariki Dunia

0
153

Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Mwinyi ametangaza kifo cha aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad.

Rais Mwinyi amesema kuwa Maalim Seif amefariki leo Jumatano Saa 5 Asubuhi katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Kufuatia kifo hicho Rais Dkt. Mwinyi ametangaza siku saba za maombolezo na kuagiza Bendera zote zipepee nusu mlingoti.