Kamati yakamilisha kazi yake TBC

0
1760

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Dkt Ayub Rioba amewataka wafanyakazi wa shirika hilo kufanya kazi wa weledi na kuwatumikia wananchi kwa kutanguliza maslahi ya shirika.

Dkt Rioba ameyasema hayo jijini Dar es salaam baada ya kupokea taarifa ya kamati ya uchunguzi wa mianya ya rushwa na upotevu wa mapato ya TBC aliyoiunda kwa lengo la kuchunguza mali na mapungufu ndani ya shirika hilo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kamati hiyo Aloysia Maneno amesema kuwa katika uchunguzi wao pamoja na mambo mengine wamebaini changamoto kadhaa zinazolikabili shirika hilo.

Kamati hiyo ya kuchunguza mianya ya rushwa na upotevu wa mapato ya TBC ilikuwa na wajumbe wanane na imefanya kazi kwa muda wa takribani wiki mbili kwa kutafuta taarifa kwa wafanyakazi na wasio wafanyakazi katika kanda ya kati Dodoma na kanda ya kaskazini katika mkoa wa Tanga.