Messi kuikabili Inter Milan

0
1866

Lionel Messi amejumuishwa kwenye kikosi cha FC Barcelona kinachosafiri hadi mjini Milan nchini Italia kuikabili Inter Milan kwenye mchezo wa ligi ya mabingwa barani ulaya.

Kujumuishwa kwa Messi kwenye kikosi hicho kumewashangaza wengi hasa baada ya ripoti ya daktari kuonyesha kuwa nyota huyo angekuwa nje ya dimba kwa kipindi cha majuma matatu baada ya kuumia mkono katika ushindi wa mabao manne kwa mbili dhidi ya Sevilla wiki mbili zilizopita.

Messi tayari amekosa michezo kadhaa ukiwemo ule wa ushindi wa mabao matano kwa moja dhidi ya Real Madrid na mchezo dhidi ya Inter Milan ambao walishinda mabao mawili kwa moja.

Kocha wa Barcelona, – Ernesto Valverde amesema kuwa hajamuondoa Messi kwenye kucheza, bali anafikiria kumrudisha kikosini mapema.

Barcelona ndiyo vinara wa kundi B wakiwa na alama tisa baada ya kushinda mechi zao zote tatu huku wapinzani wao Inter Milan wakiwa katika nafasi ya pili wakiwa wamepoteza mchezo mmoja tu dhidi ya miamba hiyo ya Hispania.