Milwaukee waendeleza ushindi NBA

0
1751

Milwaukee Bucks wameendeleza wimbi la ushindi kwenye Ligi ya kulipwa ya mpira wa kikapu nchini Marekani baada ya kuilaza Sacramento Kings alama 144 kwa 109 katika mchezo uliopigwa kwenye dimba la Fiserv mjini Milwaukee , – Wisconsin.

Licha ya Justin Jackson kuifungia Kings alama 22, bado hazikutosha kuwapa ushindi mbele ya Bucks ambao tangu kuanza kwa msimu huu wamepoteza mchezo Mmoja na kushinda michezo nane.

Katika matokeo mengine Portland Trail Blazers wameinyuka Minasota Timberwolves alama 111 kwa 81 wakati Memphis Grizilies wakinyukwa alama 102 kwa 100 na Phonix Suns.

Washngton Wizards wamechomoa na ushindi wa alama 108 kwa 95 dhidi ya New York Knicks na Philadelphoia 76’ERS wamelala kwa alama 122 kwa 97 mbele ya Brooklyn Nets.

Huko AT & T Center mjini San Antonio, -Texas, wenyeji San Antonio Spurs wameshindwa kutamba baada ya kutandikwa alama 117 kwa 110 na Orlando Magic katika mchezo ambao Aaron Gordon amefunga alama 26.

Huo unakuwa mchezo wa tatu kati ya tisa kwa Spurs kupoteza kwa msimu huu wakati Magic wakipata ushindi wao wa sita katika michezo tisa waliyocheza mpaka sasa.