Marekani kutekeleza vikwazo vipya dhidi ya Iran

0
1834

Marekani imeanza kutekeleza vikwazo vipya dhidi ya Iran katika sekta za mafuta na fedha.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, – Mike Pompeo amedai kuwa vikwazo hivyo ni vikali kuwahi kuwekwa na nchi hiyo dhidi ya Iran.

Wataalamu wa masuala ya kiuchumi wamesema kuwa, vikwazo hivyo huenda vikaathiri moja kwa moja kampuni mbalimbali zinazofanya biashara na Iran.

Mwezi Mei mwaka huu, Rais Donald Trump wa Marekani alitangaza kuiondoa nchi yake katika mkataba wa kimataifa wa nyuklia na Iran.