Cavaliers yaendelea kufanya vibaya NBA

0
2219

Cleveland Cavaliers imeendelea kupepesuka kwenye ligi ya kulipwa ya mpira kikapu nchini Marekani maarufu kama NBA baada ya kuambulia kichapo cha alama 110 kwa 91 mbele ya Denver Nuggets.

Juan Hernangomez amefunga alama 23 huku Paul Millsap akifunga alama 16 kwa upande wa Nuggets na kuwapa wakati mgumu Cleveland Cavaliers wanaoonekana kuikosa huduma ya nyota Lebron James aliyetimkia Los Angeles Lakers.

Cavaliers wanaburuza mkia kwenye kanda ya mashariki wakiwa wamepata ushindi mmoja tu kwenye michezo nane waliyoshuka dimbani kucheza.

Kwenye matokeo mengine, Philadelphia 76ERS wamewabugiza Los Angeles Clippers alama 122 kwa 113, Charlotte Hornets wamenyukwa na Oklahoma City Thunder alama 111 kwa 107 huku Atlanta Hawks wakibugizwa alama 146 kwa 115 na Sacramento Kings.

Nao Boston Celtics wamepta ushindi mwembamba wa alama 117 kwa 113 za Milwauckee Bucks ambao wamepoteza mchezo wao wa kwanza msimu huu wa NBA kwa kanda ya mashariki huku mchezo mwingine ukiwashuhudia Portland Trail Blazers wakiwafunga New Orleans Pelicans alama 132 kwa 119.