Zitto ashikiliwa na polisi

0
1853

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar Es Salaam linamshikilia mbunge wa Kigoma Mjini Kabwe Zitto.

Akizungumza na Shirika la Utangazaji Tanzania – TBC, Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar Es Salaam, Liberatus Sabas amesema jeshi hilo linamshikilia mbunge huyo kwa mahojiano kufuatia kauli anazodaiwa kutoa hivi karibuni.

Jumanne Oktoba 30 mwaka huu, Kamanda wa Polisi mkoa wa Kigoma Martin Ottieno alimtaka mbunge huyo kuwasilisha ushahidi wa taarifa alizozitoa kuwa jeshi hilo limewaua watu mia moja wa jamii ya wafugaji katika operesheni ya kuwaondoa wavamizi wa maeneo ya ranchi ya NARCO wilayani Uvinza mkoani Kigoma.