Zia ahukumiwa kifungo cha miaka saba jela

0
2039

Waziri Mkuu wa zamani wa Bangladesh na kiongozi wa upinzani nchini humo Khaleda Zia amehukumiwa kifungo cha miaka saba jela baada ya kupatikana na hatia ya kuhusika na vitendo vya rushwa.

Tayari Zia anatumikia kifungo baada ya mahakama kumpata na hatia ya kutumia vibaya mali ya umma.

Zia amesema kuwa kesi dhidi yake zimehamasishwa kisiasa kwa lengo la kumzuia asishiriki katika uchaguzi mkuu wa Bangladesh unaotarajiwa kufanyika mwezi Disemba mwaka huu.