Waendesha mashitaka wa Saudi Arabia wawasili Uturuki

0
1881

Waendesha mashitaka wa umma wa Saudi Arabia wamewasili mjini Istanbul nchini Uturuki kwa ajili ya majadiliano na serikali ya nchi hiyo kuhusiana na kifo cha mwandishi wa habari Jamal Kashoggi.

Waendesha mashitaka hao wanatarajiwa kuwasilisha ushahidi wa watu kumi na wanane wanaotuhumiwa kuhusika na kifo cha Kashoggi.

Serikali ya Uturuki inataka watuhumiwa wote kumi na wanane wanaotuhumiwa kupanga na kisha kutekeleza mauaji ya Kashoggi warejeshwe nchini Uturuki ili washitakiwe.

Serikali ya Saudi Arabia imekataa mpango huo wa Uturuki na kusisitiza kuwa watuhumiwa hao watashitakiwa na kuchukuliwa hatua za kisheria wakiwa nchini mwao.