Asasi za kiraia zatakiwa kutojiingiza kwenye siasa

0
231

Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Tanzania, Fatma Khalfan amesema tume hiyo haitakuwa tayari kufanya kazi na asasi zitakazobainika kujihusisha na siasa katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28 mwaka huu.

Baadhi ya wadau kutoka asasi za kiraia wamesema upo umuhimu wa makundi maalumu kupewa kipaumbele zaidi ikiwemo wanawake, wazee na watu wenye ulemavu katika zoezi zima la uchaguzi mkuu.