WALIOCHUKUA FOMU HII LEO

0
326

Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango akionesha fomu ya kuwania kuteuliwa kugombe ubunge Jimbo la Buhigwe Mkoa wa Kigoma kupitia CCM. Mbunge anayemaliza muda wake wa jimbo hilo ni Albert Obama wa CCM.



Waziri wa Uwekezaji, Angellah Kairuki amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea ubunge Jimbo la Same Magharibi kupitia Chama cha Mapinduzi. Anayemkabidhi fomu hiyo ni Katibu wa CCM Wilaya ya Same, Victoria Mahembe.

Naibu Spika wa Bunge la Tanzania, Dkt. Tulia Ackson amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya kuteuliwa kuwania nafasi ya Ubunge wa Jimbo la Mbeya Mjini kupitia CCM. Dkt.Tulia amechukua fomu hiyo leo katika Ofisi za CCM Wilaya akisindikizwa na mume wake, James Mwainyekule.


Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo, leo amechukua fomu za kuomba ateuliwe kugombea ubunge katika Jimbo la Arusha Mjini, kupitia Chama cha Mapinduzi.
Waziri wa Viwanda na Biashara Innocent Bashungwa amechukua fomu katika Ofisi ya CCM Wilaya ya Karagwe kutetea uwakilishi wa jimbo la Karagwe Kupitia Chama Cha Mapinduzi.
Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Monduli, Langael Akyoo, leo Jumanne July 14,2020 amemkabidhi Fredrick Lowassa fomu ya kuomba ridhaa ya Chama hicho ya kugombea Ubunge wa Jimbo la Monduli, Fredrick ni Mtoto wa Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof Joyce Ndalichako, amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kimteue agombee ubunge katika Jimbo la Kasulu Mjini mkoani Kigoma.
Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Ilemela ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ardhi, Dkt. Angelina Mabula leo amechukua fomu ya kutetea kiti chake cha ubunge katika Ofisi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) wilayani Ilemela.